Tuesday, March 3, 2020

LIACHE CHOZI LANGU : Sehemu ya 4




SEHEMU YA NNE
WATUNZI wastara juma, @hadithizetu
Whatsapp 0769510060
Mke wa millaji alikataa katakata mimi kukaa pale kwake, hakuwa na huruma hata kidogo, “weee siwezi kukubali kuharibu ndoa yangu, mimi sitaki lawama Wastara, wewe ondoka Mungu atakusaidia maisha yako mbele kwa mbele” alisema yule mke wa millaji bila hata huruma.
Niliamua kuondoka nikiwa nachechemea maana kile kidonda kilikuwa bado kinauma sana, niliondoka bila kujua naenda wapi, ikabidi niende palepale nyumbani palipo ungua ili nitulize akili, kibaya zaidi kipindi nipo pale maeneo ya nyumbani mvua ikaanza kunyesha nikiwa na mtoto na nikiwa naumwa, sikuwa na pesa japo ya kununua hata poda, sabuni na mahitaji mengine ya mtoto.
Niliamua kwenda mpaka kwa mdogo wangu ili japo wanisaidie, kumbe na yeye pia alikuwa anakaa na mme wake chumba kimoja hivyo mambo yalikuwa bado magumu kwangu, shemeji alinionea huruma ingawa bado alikuwa bado anaumwa akanipa pesa ya kukaa chumba cha wageni (guest house), nilitafuta sehemu na kweli nikapata, sasa wakati nipo pale gesti, kumbe kwa nje walikuwa wanauza pombe na yule mwenye gesti alikuwa amelewa pia, kipindi namuita ili niweze kumlipa hela akawa hasikii kabisa, nilipo mfata anipe chumba akasema vimeisha lakini atanisaidia sehemu ya kulala, sikuweza kukataa maana nilikuwa nimechoka sana kumbeba mtoto mpaka mikono ikawa inauma hapo sijala chochote, sijaoga, sijanywa dawa nilizo kuwa nazo.
Yule baba alinipa chumba ila alicho nishangaza eti na yeye akaja kulala humohumo chumbani, niliogopa nikajua hapa lazima nibakwe tena, yule baba alilala akiwa amelewa huku mimi nimekumbatia mwanangu, sikupata usingizi kabisa kwa woga kwamba nitabakwa, yule baba kuna mda alianza kunipapasa nikashtuka, “naomba tufanye mapenzi nitakulipa” alisema yule baba akiwa amelewa sana, niliogopa kumbemenda mtoto, ndipo nikaamka ili nitoroke, kumbe alikuwa amefunga mlango alafu funguo kazificha, ilibidi nimlaze mtoto kwa chini maana nilitandika nguo zilizo kuwepo pale ili mtoto asiumie, ndipo nikarudi kitandani ili nimuelezee yule baba hali kiafya asinifanyie lile tendo, yule baba akanibembeleza sana kwamba yupo tayari hata kunioa nikubali kufanya nae mapenzi.
Nilikataa katakata lakini kutokana na pombe za yule baba, bila kujua akanivuta kwa nguvu ili nivue nguo tuweze kufanya tendo, lakini kumbe akawa ameshika na kukitonesha kidonda nilicho fanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua, maumivu yalikuwa makubwa sana, damu zikaanza kunitoka, ndipo yule baba akaanza kupagawa akajua kwamba tayari ameua maana nilidondoka chini kutokana na yale maumivu ya tumbo, ndipo yule baba akaamua kunibeba mzima mzima kisha akaenda kunilaza nje kwa mbali kabisa na pale gesti kwake, baada ya mda huku nikiwa nasikia uchungu tumboni ambao nisingeweza hata kuongea chochote nikaona amemleta mtoto wangu akiwa analia usiku wa manane.
Nilishindwa kabisa kumbembeleza mtoto asilie, maana maumivu niliyo kuwa nasikia yalikuwa makali sana, sasa basi kutokana na sauti ya mtoto kuna watu walikuwa wanapita hao watu walikuwa wa ajabu na hata nguo walizo kuwa wamevaa zilikuwa kama za kichawi yaani washirikina, hivyo basi walipo muona mtoto wangu ambae alikuwa bado ni mchanga, wakataka kumchukua ili wakamtumie kama dawa ya mambo yao ya kishrikina, wakati huo sina nguvu wala chochote cha kuweza kujitetea ili nikomboe uhai wa mwanangu nilie mzaa kwa shida.
USIKOSE SEHEMU YA 5
WATUNZI WASTARA JUMA, @hadithizetu
Whatsapp 0769510060

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only